Blogger Widgets

Tuesday, 10 December 2013

Tanesco kupandishwa kortini Mahakama Kuu


Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) leo linafikishwa katika Mahakama Kuu na Kampuni ya MacDonald Live Line Technology likidaiwa fidia baada ya kusitisha mkataba wa kukarabati njia ya umeme kati ya Mikoa ya Arusha na Kilimanjaro.
Kampuni hiyo ambayo imekuwa ikikarabati na kusafisha njia za umeme bila kuuzima, imeamua kuchukua hatua hiyo baada ya Tanesco kuishinda katika usuluhishi wa mgogoro na kusitisha mkataba huo.
Meneja Uhusiano wa Tanesco, Badra Masoud alipopigiwa simu jana ili kuzungumzia suala hilo, mara kadhaa alijibu kwa kifupi kuwa alikuwa akiendesha gari hivyo asingeweza kuzungumza na simu.
Mkurugenzi wa MacDonald Live Line Technology, Macdonald Mwakamele alisema msuluhishi wa mgogoro huo aliipa ushindi Tanesco na kuitaka MacDonald kulipa gharama kwa shirika hilo kama fidia na usumbufu uliotokana na kutokamilisha kazi iliyopewa katika mikoa hiyo
Alisema kampuni hiyo ilipeleka malalamiko yake kwa msuluhishi, Wakili Mtango Jonathan Lukwalo, baada ya Tanesco kusitisha mkataba kwa kampuni hiyo kwa madai kuwa ilichelewa kutekeleza kazi ya ukarabati wa njia za umeme mkoani Arusha.
Mwakamele alisema Tanesco na kampuni hiyo waliingia mkataba Machi mwaka 2010 wa kufanya ukarabati wa njia ya umeme njia ya Kilimanjaro-Arusha kwa kutafuta nguzo, kuzisafirisha kwenda eneo la kazi.
Alisema kazi hiyo ilitakiwa kukamilika ndani ya wiki 32 kuanzia Julai 2010, 28 hadi Machi 9, 2011.

No comments:

- See more at: http://www.helperblogger.com/2012/06/jquery-facebook-like-box-popup-with.html#sthash.AGJhd6Gy.dpuf