
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, limefanya kikao cha dharura kuhusu Sudan Kusini, baada ya wanajeshi wa Umoja huo kuuawa katika ghasi nchini humo.
Wanajeshi watatu wa kulinda amani wa Umoja wa
Mataifa kutoka India, waliuawa nchini Sudan Kusini katika shambulio
lililotokea kwenye kambi ya Umoja wa Mataifa.
Mauaji hayo yalifanyika wakati ambapo mapigano
kati ya vikosi vya waasi na majeshi ya Serikali yakiongezeka, hali
inayozusha wasiwasi wa nchi hiyo kuingia katika vita vya wenyewe kwa
wenyewe.
Balozi wa India katika Umoja wa Mataifa, Asoke
Mukerji alisema wanajeshi hao wameuawa katika shambulio lililofanywa na
vijana wa kabila la Nuer kwenye kambi ya Akobo, jimbo la Jonglei.
Wakati huohuo, Marekani imepeleka wanajeshi 45 Sudan Kusini ili kuwalinda raia wake na mali zao.
Wanajeshi hao watabakia Sudan Kusini hadi usalama
utakapoimarika. Rais wa Marekani, Barack Obama alitoa wito mapigano hayo
kusitishwa mara moja, akionya nchi hiyo inaweza ikatumbukia katika
vita.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Farhan Haq alisema “Mapigano yametokea na hatujathibitisha hali ilivyo’’
Alisema Tume ya Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS itaondoa wafanyakazi wake wasiyo wa kijeshi kutoka Akobo.
Habari nyingine zinasema, wafanyakazi wenyeji 14
wa kampuni ya mafuta nchini Sudan Kusini wameuawa katika mapigano kati
ya makundi ya wapiganaji kutoka makabila ya wa Dinka na wa Nuer.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon
ametaka kufanyike mazungumzo ya kisiasa ili kulinusuru taifa hilo ambalo
bado ni changa.
Katika taarifa yake, kiongozi huyo wa Umoja wa
Mataifa alisema hatma ya taifa hilo changa ipo katika mikono ya uongozi
wake wa sasa ambao unapaswa kufanya kila liwezekanalo kudhibiti
machafuko ambayo yatakuwa usaliti mkubwa kwa zile jitihada za muda mrefu
za kutafuta uhuru wake.
Alisema viongozi wa nchi hiyo wanatakiwa kudhihirisha uhuru wao waliopata kwa kuutafuta kwa muda mrefu ambapo walifanikiwa.
Raia wa nchi hiyo mpaka sasa wamekosa amani kwani wanahaha kutafuta pa kukimbilia huku wakitafuta msaada kutoka nchi jirani.
Raia wa nchi hiyo mpaka sasa wamekosa amani kwani wanahaha kutafuta pa kukimbilia huku wakitafuta msaada kutoka nchi jirani.
No comments:
Post a Comment