Blogger Widgets

Friday, 18 October 2013

Aliyetekwa Moshi ni mkwe wa kigogo Dar

Moshi. Mambo mazito yameibuka kufuatia tukio la kutekwa nyara kwa mwanamke mmoja wa mjini Moshi wiki iliyopita.
Mambo hayo ni pamoja na kubainika kuwa aliyetekwa ni mke wa mtoto wa kigogo mmoja wa Serikali mkoani Dar es Salaam.
Mwanamke huyo aliyesafirishwa na watekaji hadi jijini Dar es Salaam ni mke wa mfanyabiashara Jerome Mushi ambaye ni mtoto wa Mkuu wa Wilaya ya Ilala iliyoko mkoani Dar es Salaam, Raymond Mushi.
Taarifa za uhakika zilizopatikana jana zilisema watekaji hao akiwemo mwanamke mmoja waliojifanya kuwa ni maofisa wa upelelezi wa polisi, waliondoka na kitita cha Dola 11,000 sawa na Sh18 milioni.
Habari hizo zinadai kuwa baadaye mwanamke huyo aliahidi kuwalipa watekaji hao Sh100 milioni lakini angezilipa fedha hizo jijini Dar es Salaam kupitia kwa mtu anayetajwa kwa jina la utani la White.
“Aliwaambia atawapa Sh100 milioni na kwamba katika akaunti yake kuna Sh30 milioni na walisafiri naye hadi Dar es Salaam kwa kutumia gari la watekaji aina ya Toyota.
RAV4,”kilidokeza chanzo chetu.
Ilielezwa kuwa baada ya kufika jijini Dar es Salaam Ijumaa iliyopita, mwanamke huyo pamoja na watekaji wake walifikia katika hoteli moja na kumpigia simu White ili amnasue katika jambo hilo.
Hata hivyo, White inadaiwa alitilia mashaka uhalali wa polisi hao na akauliza kwa baadhi ya polisi anaowafahamu ambao walimjulisha kuwa watu hao ni mtandao wa genge la matapeli wa jijini.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz amethibitisha habari kuhusu kutekwa nyara kwa mwanamke huyo.
“Ni kweli hao watu walifika nyumbani kwa huyo mwanamke na kujitambulisha kuwa ni maofisa wa polisi wakimtuhumu
kuwa anajihusisha na biashara ya dawa za kulevya,”alisema Kamanda.

Kamanda Boaz alisema baada ya mumewe kurudi nyumbani na kuelezwa kuwa mkewe amepelekwa Kituo cha Polisi mjini Moshi, alifuatilia ili kujua kulikoni.
Alisema hata hivyo walimweleza kuwa hakuna shauri la aina hiyo.

No comments:

- See more at: http://www.helperblogger.com/2012/06/jquery-facebook-like-box-popup-with.html#sthash.AGJhd6Gy.dpuf