Klabu ya Tottenham Hotspurs imekubali kuilipa Valencia ya Hispania kiasi cha Euro Milioni 30 kwa ajili ya mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania Roberto Soldado . Hii ni baada ya klabu hizo mbili (Valencia & Tottenham) kufikia makubaliano katika mazungumzo yaliyofanyika hapo jana (siku ya jumamosi).
Mkurugenzi wa masuala ya ufundi wa Tottenhma Mtaliano Franco Baldini alikuwepo jijini Valencia kukamilisha mazungumzo hayo ambapo Spurs wanatarajiwa kumthibitisha Soldado kama mchezaji wao rasmi baadaye wiki inayofuata .
Usajili wa Soldado unamfanya kuwa mchezaji wa tatu kusajiliwa na Spurs baada ya kiungo wa Brazil Paulinho aliyesajiliwa toka klabu ya Corinthians na Winga wa Ubelgiji Nacer Chadli toka klabu ya Fc Twente ya Uholanzi.
Roberto Soldado anakaribia kukamilisha usajili wake ndani ya Tottenham Hotspurs siku chache zijazo.
Tayari Spurs imekamilisha mazungumzo ya masuala binafsi na mchezaji mwenyewe(Soldado) na kilichobaki ni kukamilisha jinsi malipo yatakavyofanyika baina ya klabu mbili ambapo Valencia wangependa kulipwa kwa mikupuo miwili ya Euro milioni 15 huku Spurs wakijaribu kufanya malipo hayo kwa mikupuo mingi kwa nyakati tofauti .
Kiungo mpya wa Spurs Paulinho aliyesajiliwa toka Corinthians .
Nacer Chadli Mbelgiji mwenye asili ya Moroco aliyesajiliwa na Spurs toka Fc Twente.
No comments:
Post a Comment