Blogger Widgets

Wednesday, 27 November 2013

BALE:kabla sijatua Madrid nliomba ushauri kwa Beckham


SUPASTAA, Gareth Bale, amefichua kwamba alimtwangia simu staa David Beckham kuomba ushauri kabla ya kuchukua uamuzi wa kujiunga na Real Madrid katika usajili uliopita wa majira ya kiangazi.
Staa huyo wa kimataifa wa Wales alivunja rekodi ya Cristiano Ronaldo ya uhamisho baada ya kujiunga na Los Blancos kwa ada ya Pauni 86 milioni Septemba mwaka huu.
Winga huyo wa zamani wa Tottenham Hotspurs, alisema alipata ushauri kutoka kwa Beckham aliyewahi kung’ara na timu hiyo ya Hispania na alimfundisha namna ya kuhimili maisha ya Hispania.
Alipoulizwa ni wachezaji gani amekuwa akiwasiliana nao, Bale alisema: “Wote. David Beckham alinitumia meseji ya kunitakia heri na mambo mengine. Lilikuwa jambo zuri sana na nimefurahi.
“Alifanya mazoezi Tottenham tukiwa pamoja kwa muda fulani, hivyo namfahamu vizuri na nimekuwa nikimtumia meseji na kumpigia simu.
“Namfahamu Jonathan Woodgate pia na nimekuwa nikifanya naye mawasiliano. Nilikutana pia na Steve McManaman kwenye mahojiano na tulizungumza mengi sana.”

No comments:

- See more at: http://www.helperblogger.com/2012/06/jquery-facebook-like-box-popup-with.html#sthash.AGJhd6Gy.dpuf