
Mkurugenzi wa jiji la Arusha Sipora Liana akiwa anaongea na waandishi wa habari kuhusiana na uchaguzi wa udiwani jijini hapa

picha chini na juu waandishi wa habari wakiwa wanasikiliza mkurugenzi wa jiji la Arusha


Halmashari ya jiji la Arusha inatajia kufnya uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata nne za jijini hapa
ambazo ni Elerai ,Kaloleni ,Kimandolu pamoja na Themi mnamo july 14
mwaka huu uchaguzi huu mdogo unafanyika kutokana na kuairishwa kwa
uchaguzi mdogo wa kata hizi katika jimbo la Arusha mjini kutokana na
sababu za kiusalama.
Akiongea na waandishi wa habari mkutugenzi wa jiji la Arusha Sipora Liana alisema kuwa uchaguzi
huo uliarishwa kutokana Juni 16 kutokana na mabomu yaliyopigwa siku
moja kabla ya uchaguzi na mungine ukaarishwa mapema juni 30 kutokana na
kutojiridhisha kwa hali ya usalama iliyokuwepo katika jiji la Arusha.
Alisema
kuwa kwa sasa maandalizi yaote yamekamilika na taratibu zote za
kutangaza tena kwa wasimamizi ,wasimamizi wasaidizi pamoja na makarani
zimekamilika na pia wameshapatiwa mafunzo kwa ajili ya wasimamizi hawa yameanza jana na yataendeshwa kwa muda wa siku tatu.
Aidha
Sipora alisema kuwa jumla ya wasimamizi waliochaguliwa kusimamia
uchaguzi ni 416 ikiwemo wasimamizi wa vituo 136 ,wasimamizi wasaidizi
135 ,makarani 136 pamoja na wasimamizi wa akiba wakiwa nane..
Pia
aliwataja wananchama walioteuliwa kugombea nafasi za udiwani kuwa ni
pamoja na Mwl.Emmanuel Micheel Laizer (ccm),Gilbert Bayo(CUF),Seif
Shimba (CCK),Eng Jeremiah Mpiga (CHADEMA) Boidafi shirima (TLP) hawa
wakiwa ni wagombea wa kata ya Elerahi ,wagombea wa kata Kaloleni ni
pamoja n Emmanuel Miliari (CCM) ,Darwesh Ramathani (CUF),Kessy
Lewi(CHADEMA) pamoja na Ngilisho Pauli kutoka chama cha demokrasia
makini ,waonao toka kata ya Themi ni pamoja Victoro Mkolwe (CCM),kinabo
Edmound(CHADEMA) na Lobora Ndaproi (CUF) .
Aliwataja wagombea kutoka kata ya Kimandoku ni pamaja Edna Saul
(CCM) pamoaja na Rayson Ngowi kutoka (CHADEMA) ,aidha alisema kuna
jumla ya vituo 136 vya kupigia kura ambapoalisema kaloleni kuna vituo
27,elerahi 55,kimandolu 39, na kata ya themi vituo 15 .
Alisema kuwa jumala ya wapiga kura sitini elfu mia moja
ishirini na tatu (60,123)wanatakiwa kupiga kura kaloleni itakuwa na
wapiga kura 12,636,Elerai watakuwa wapiga kura 23,797,kimandulu 17,294
na Themi wapiga kura 6,396 aidha alisema kuwa wapiga kura wote
wanatakiwa kufika katika vituo mapema kwani kura zitaanza kupigwa kuanzia saa moja asubui hadi saa kumi jioni ambapo baada ya hapo watafunga na askari watakuwa wanalinda vituo vyote.
Aliwataka
wananchi kutimiza wajibu wao wa kupiga kura kwani zoezi hili ni muhimu
huku akiwahakikishia kuwa usalama utakuwepo wa kutosha wakati wa kupiga
kura na aliwataatharisha wananchi kuwa endapo
mtu yeyete atawasumbua wakiwa katika eneo la kupigia kura watoe taarifa
kwa askari aliopo karibu yake ili achukuliwe hatua za kisheria.
''ninawaomba
kutowazingatia wanaopita kuwaaambia msijitokeze kwenda kutumia haki
yenu ya msingi za kikatiba kuwachagua viongozi wenu pia napenda
kuchukuwa nafasi hii kuwatakia wananchi wote wa jiji wa arusha uchaguzi mwema''alisema Sipora.
No comments:
Post a Comment